Wednesday, March 2, 2016

AFUNGWA JELA MIAKA 20 KWA UJANGILI



Chanzo: Gazeti la Raia Tanzania, Machi 1, 2016

Kibaha: Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Pwani imemuhukumu mfanyabiashara Anania Betela (30) amehukumiwa kwenda jela miaka 20 na kulipa faini ya Sh.1.9 bilioni baada ya kupatikana na hatia katika kesi ya kukutwana vipande 28 vya meno ya tembo bila kibali.
Picha ya Tembo wakiwa katika moja ya mbuga za wanyama za Tanzania
 
Mshtakiwa huyo alihukumiwa terehe 29 Februari 2016, mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Herieth Mwailolo, aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo huku upande wa mashtaka ukiwakilisha na Wakili wa Serikali, Salim Msemo.
Akitoa adhabu hiyo Hakimu alisema, mshtakiwa alikuwa akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba moja ya mwaka 2014.

Katika kesi hiyo mshtakiwa anadaiwa kutenda kosa mwaka 2014 eneo la Vigwaza, wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani ambapo alikutwa na vipande hivyo vya meno ya tembo vyenye thamani ya shilingi milioni 198.
Upande wa mashtaka ulikuwa na jumla ya mashahidi watano Pamoja na vielelezo mbalimbali ikiwemo men ohayo, begi lililobeba meno hayo katika kuthibitisha kesi dhidi ya mshtakiwa.
Baadhi ya meno ya Tembo yaliyo wahi kukamatwa kutokana na ujangili


JICHO LA PILI

Ujangili unapaswa kupigwa vita, wananchi tunawajibu wa kuhakikisha kuwa tunasimamia na kulinda rasilimali za Taifa kwa ajili ya maendeleo yetu na vizazi vijavyo. Vitendo hivi vimekithiri na vinalisababishia taifa hasara kubwa, ni biashara inayo nufauisha watu wachache. Hebu tujiulize uvunaji huu wa kasi wa tembo, usipo pingwa, baada ya miaka kumi hali itakuwaje?

Je, kutakuwa na tembo hata mmoja? Vipi kuhusu biashara ya utalii, itakuwepo?
Ripoti ya Taasisi ya Kulinda Tembo (TEPS) ya mwaka 2015 inaonesha kuwa asilimia 60 ya Tembo waliuawa kuanzaia mwaka 2009 mpaka mwaka 2014. Mwaka 2009 kulikuwa na Tembo 109,051 na ni Tembo 43,330 ndio waliokuwa wamesalia hadi mwaka 2014. Pia ripoti inaonesha kuwa tembo 61,720 waluiawa kwa miaka mitano mfululizo ikiwa ni wastani wa Tembo 30 kwa siku.

Ukweli ni kwamba Tembo hao wakiwa hai wanaliongezea taifa mapato makubwa kupitia biashara ya utalii kuliko wanapo uawa na kuuza meno yao.

Idadi ya Watalii imekuwa ikiongezeka kila mwaka hii inaonesha kuwa sekta ya utalii inakua na kukuza uchumi wanchi hivyo kila mwananchi ana wajibu wa kupinga ujangili wa wanyamapori wetu.

Pinga Ujangili, Okoa Tembo wa Tanzania!

No comments:

Post a Comment