Wednesday, October 27, 2010

ATHARI ZA MAZINGIRA ZILETWAZO NA UPANDAJI MITI KATIKA MASHAMBA MAKUBWA

Article By Joyceline Kobero,
Legal Officer
Lawyer's Environmental Action Team (LEAT)

ATHARI ZA MAZINGIRA ZILETWAZO NA UPANDAJI MITI KATIKA MASHAMBA
MAKUBWA
UKAME
Mabadiliko ya tabia nchi yamekuwa yakisababishwa hasa na kuongezeka kwa kiasi kikubwa cha matumizi ya nishati Kaskazini, lakini athari zake zitasikika/onekana zaidi Kusini. Uwiano huu usiolingana utaendelezwa na [gesi ya kaboni dioxide iliyohifadhiwa ambayo ina madhara kwa mazingira] kwasababu kiwango kikubwa cha upandaji wa miti itakuwa inapandwa Kusini ambapo kuna ardhi,nguvu kazi ya gharama nafuu, lakini ambapo jamii za kienyeji wamepewa nafasi finyu kushiriki katika majadiliano ya hali ya hewa. 
MAFURIKO
Tatizo la mabadiliko ya tabia nchi ambayo ulimwengu unaukabili linajulikana vizuri na pia suluhisho. Mkusanyiko wa gesi ya janikiwiti katika hewa ni matokeo ya vitendo vya uzalishaji na matumizi yasiyo na tija. 
Moja kati ya gesi muhimu ya janikiwiti ni kaboni dioxide. Sehemu kubwa ya utoaji wa gesi hii shina lake ni vyanzo vikuu viwili: matumizi ya mafuta na gesi kutoka chini ya ardhi na mlolongo wa ukataji miti (ambayo inaruhusu kutolewa kwa kaboni iliyohifadhiwa katika ujumla wa viumbe hai-biomass). Kwahiyo tiba/suluhisho ni kuondoa matumizi ya mafuta na gesi kutoka chini ya ardhi na kuzuia ukataji miti. 
Swali si kama ufumbuzi wa tatizo utafanikiwa sasa ila kwa vyovyote vile serikali zinaonyesha mapatano ya kufikia kusudi/madhumuni na ufumbuzi unatekelezwa kabla ya mfumo wa ikolojia wa dunia na jamii haujaangamia kabisa. Upandaji miti,unaotangazwa kama moja ya suluhisho muhimu kwa mabadiliko ya tabia nchi, wenyewe uko wazi/hatarini zaidi kwa kufyekwa/kukatwa katika nchi nyingi, ambapo misitu imekuwa mbadala wa kilimo cha aina moja ya shamba kubwa la miti. Wakati huo huo suluhisho hili linasababisha matatizo zaidi kwa mahali pale na mazingira, kwa kuwa wenyeji
wanahamishwa{matokeo yake ni ongezeko la ukataji miti], rasilimali udongo na maji zinapungua sana na makazi ya wanyama na mimea inaondoshwa/futika, kutaja kwa uchache.
UVUNAJI WA MAGOGO

Mashamba makubwa ya miti kwa mtazamo wetu.si misitu; mashamba ya miti ina kitu kimoja tu na misitu: kuna miti. Lakini, kimsingi vinatofautiana. Msitu ni changamani,ina utaratibu/mfumo wa kujiotea wenyewe,inajumuisha udongo,maji,mabadliko kidogo ya tabia nchi,nishati, na aina mbalimbali za mimea na wanyama katika uhusiano wa pamoja. Mashamba ya kibiashara,kwa upande mwingine, ni sehemu inayolimwa ambayo aina ya mimea na muundo vimerahisishwa kuvutia kuzalisha bidhaa chache ,kama magogo, makaa,utomvu, mafuta au matunda. Shamba la miti tofauti na msitu,lina aina ndogo ya mimea na umri, na linahitaji muingiliano wa kila siku kwa sehemu kubwa na binadamu.

Mashamba ya miti yanakaribiana kwa karibu na kilimo cha mazao ya viwandani kuliko msitu ambao kama kawaida unaeleweka au shamba la kilimo la asili. Kama kawaida mashamba makubwa ya miti yanategemea maelfu au hata mamilioni ya miti ya aina moja,inayozalishwa kwa ukuaji wa haraka, umoja na mavuno makubwa ya malighafi na inapandwa katika mistari inayolingana,inahitaji maandalizi ya kutosha ya udongo,mbolea,kupanda kwa kuacha nafasi,uchaguzi wa mbegu,kupalilia magugu kwa kutumia mashine au sumu ya mimea,matumizi ya dawa ya kuulia wadudu, embamba, kuvuna kwa mashine na wakati mwingine kupogoa.
ATHARI KWA WANYAMA

Tofauti haikwepeki- mashamba ya miti si msitu na kitu kimoja kinachofanana ni kwamba vote viwil,miti ndo inatawala kwa muonekano wa mara moja. Hapo kufanana kunaisha. Mkataba wa makubaliano Kyoto, wa Disemba 1997 ulikosolewa kwa mtazamo wake wa kisoko, kwa sababu ulilenga kuanzisha mfumo wa kibiashara wa kununua na kuuza utokezaji wa kaboni. Upandaji wa miti umeongeza wajibu mkuu kuhusiana na jambo hili kwa sababu ya dhana yao ya masharti ya uhifadhi wa kaboni (kaboni sinki- ni hazina ambayo inaweza kufyonza au kutenga kaboni dioxide kutoka kwenye angahewa pamoja na misitu,udongo,maji ya bahari na mabaki yenye kaboni katika kina cha bahari).

Katika makubaliano ya Kyoto, Marekani wameweka mkakati wa kudhibiti kuongezeka kwa gesi za janikiwiti kwa kuanzisha soko la kimataifa la uhifadhi wa kiwango cha kaboni. Ili utengenezaji wa kiwango cha utoaji wa kaboni ulete utaratibu wa maana, vipimo vya upunguzaji wa kaboni na uhifadhi vitahitaji kuwa vya wastani/aina moja. Njia ya uvumbuzi wa kaboni inahusisha kiwango cha chini cha kaboni iliyopo sehemu husika, na kuanzisha sehemu za mfano za kudumu za viwanja, na kukagua kila baada ya vipindi Fulani uoto wa mimea wa eneo na maeneo mengine. Utengenezaji wa kaboni, ni utoaji wa kibiashara mahsusi kwa kaboni dioxide. Ni moja ya njia ambazo nchi zinaweza kutimiza wajibu wao chini ya makubaliano ya Kyoto kupunguza utoaji wa kaboni ili kujaribu kupunguza ukali wa mabadiliko ya tabia nchi kwa siku zijazo.

Biashara ya utoaji kaboni hufanya kazi kwa kuuza kiasi fulani cha utoaji wa kaboni inayozalishwa na mtoaji. Utoaji wa gesi za janikiwiti unaathiri ustawi wa watu wanaoishi siku zijazo, na pia kuathiri mazingira halisi. Ulimwengu mzima kumekuwa na majaribio mengi ya kuanzisha miradi ya kupunguza kaboni kwa kutumia upandaji miti wa kiwango kikubwa kama njia ya kufyonza kaboni,kwa madhumuni yaliyoainishwa ya kupunguza hewa ya ukaa,ambayo inafikiriwa kuwa ni sababu kubwa ya kuongezeka kwa joto na mabadiliko ya tabia nchi. Ingawa upandaji miti kwa kiwango kikubwa umejumuishwa kwa pamoja katika utaratibu wa maendeleo safi wa makubaliano ya Kyoto,lakini bado hakuna uwezekano wa kuzalisha uhifadhi wa kaboni kwa njia ya kuanzisha mashamba ya miti kwa sababu mbalimbali. Moja ya kikwazo kikubwa cha wazi/kueleweka ni kwamba mashamba ya miti ni mazao ya muda ya mbao, ambayo kawaida hukatwa kwa ajili ya mbao za karatasi au mbao ndani ya kipindi cha muda mfupi; na ipo katika hatari kubwa ya kushika moto na kwa asili yake pia ipo hatarini kwa kiwango cha juu kuharibiwa na magonjwa,upepo na ukame.

Matokeo yake, miti michache ndo itaweza kufaa kuhifadhi kaboni kwa vipindi virefu zaidi kutosha kupunguza ukali wa mabadiliko ya hali ya hewa has ukiangalia madhara ya mabadiliko ya hali ya hewa katika mashamba makubwa.
Mashamba makubwa ya miti yenyewe hayana uzuri au ubaya:kama kuna manufaa au madhara/hatari inategemea na ukubwa wake, lengo lililokusudiwa na aina ya miti,pamoja na mazingira ya asili,kijamii na uchumi mahali yanapoanzishwa. 
Lakini kwa mazingira ya makubaliano ya Kyoto,mamilioni ya hekari za ardhi zitakuwa zimechukuliwa kwa ajili ya kutwaa kaboni ili kuwa na madhara kidogo katika jumla ya utoaji(kupunguza utoaji). Matokeo ya utafiti yanalenga kuongeza ufahamu miongoni mwa wawakilishi wa serikali kuhusu matatizo ya kijamii na kimazingira ambayo yatatokea kutokana na uanzishwaji wa mashamba makubwa ya miti kuhifadhi kaboni, ili waweze kuchukua uamuzi rasmi kulingana na jambo hili.

Moja ya madhara yaliyo wazi ya upandaji wa miti ni maisha ya mashaka kati ya jamii na bahari ya mashamba ya mbao ambayo yanapunguza fursa ya kutumia ardhi kwa kulima na kufuga, ilhali kuna manufaa kidogo ya moja kwa moja katika ajira na mambo mengine ya kijamii na kiuchumi. Jamii inajisikia kutengwa sana na haya mashamba makubwa ya mbao. Kupotea kwa mimea na
wanyama wa eneo husika kutokana na mashamba hayo kuna hatari kijamii,kitamaduni na kiuchumi kwa jamii kwa ujumla.

Mashamba ya mbao za viwandani mara zote huwa na matokeo hasi kwa jamii za kienyeji,uchumi na viumbe hai. Mabadiliko ya matumizi ya ardhi yanaathiri watu na riziki yao, na kwa upande mwingine zinaathiri utoaji wa gesi ya janikiwiti. Hili ni eneo ambalo lkwa kiasi kikubwa limesahaulika au kudharaulika na linaweza kusababisha utoaji wa gesi ya janikiwiti kwa kiwango ambacho hakijawahi kuandikwa ambayo yanatokana na mashamba ya ya miti yanayozalisha na kuhifadhi kaboni. Wenyeji na jamii husika zinazoishi katika misitu wanateseka kwa kuingiliwa/kutwaliwa kwa ardhi yao na makampuni ya mashamba na wanalazimika kuyaacha,kupoteza ardhi yao na riziki, hii inamaanisha kudharau msingi wa kiini na kiroho wa tamaduni zao . Katika mifano mingi,mashamba makubwa yanahitaji uharibifu wa misitu ya asili ambayo hatimaye huathiri asili ya kazi/riziki.

Ndio,wanatoa ajira kwa jamii husika kama wafanyakakzi wa mashambani(lakini mara zote na kwa vipindi) na baadae wanahamia sehemu zingine kwasababu mashamba yanatoa nafasi chache za ajira kuliko shughuli za kilimo ambazo ni mbadala. Kwa kiasi kikubwa, wanaonekana kama chanzo cha wafanyakazi wa bei rahisi wakayti wa kupanda na baadae , wakati wa kuvuna miti.

Hii inamaanisha kwamba kabla mashamba makubwa ya miti hayajawa hifadhi ya muda ya kaboni, ukweli ni kwamba yana sababisha kutolewa kwa kiasi kikubwa cha kaboni ambayo awali ilihifadhiwa katika misitu na udongo wa msituni unachukua nafasi wakati mashamba makubwa ya miti inapotokea.
Mabadiliko ya tabia nchi yamekuwa yakisababishwa hasa na kuongezeka kwa kiasi kikubwa cha matumizi ya nishati Kaskazini, lakini athari zake zitasikika/onekana zaidi Kusini. Uwiano huu usiolingana utaendelezwa na [gesi ya kaboni dioxide iliyohifadhiwa ambayo ina madhara kwa mazingira] kwasababu kiwango kikubwa cha upandaji wa miti itakuwa inapandwa Kusini ambapo kuna ardhi,nguvu kazi ya gharama nafuu, lakini ambapo jamii za kienyeji wamepewa nafasi finyu kushiriki katika majadiliano ya hali ya hewa.
 
Upandaji wa miti una athari katika maeneo mengi ya mazingira ikiwemo maji. Mazao yote yanafanya kazi kama mabomba ya kuvutia maji, ni kwamba virutubisho vya udongo vinafikia majani yaliyoyeyushwa kwenye maji. Jinsi ukuaji unavyokuwa wa haraka,ukubwa wa mmea na ukubwa wa eneo na ndivyo kiwango kikubwa cha maji yanatumika. Inapunguza mtiririko wa maji, utoaji wa maji ya ardhini na ubora; zikiambatana na athari za viumbe asili vya majini.

Udongo pia unaathirika.Mashamba makubwa yanasababisha mabadiliko katika muundo wa udongo na mchanganyiko wa kemikali, ikihusisha na utumiaji wa mashine nzito zinazoweka mmomonyoko wa udongo. Virutubisho muhimu vinatolewa wakati magogo yakiondolewa. Mabadiliko haya kwa kiasi kikubwa hayabadiliki. Athari katika mfumo wa ikolojia ya mahali: kwa kuwa sehemu kubwa ya wanyamapori,mashamba hayatoi chakula wala malazi wala fursa ya kuzalisha. Pia zina athari kubwa katika vitu vinavyohusiana na ikolojia ya mkoa kama ukanda wa mbuga, eneo chepechepe na vyanzo vya maji.

Sunday, October 10, 2010

VYURA WA KIHANSI: THAMANI YA MALIASILI DUNIANI


Article by Heri Ayubu ,LL.B (Hons)  
Environmental Lawyer,
Lawyers’ Environmental Action Team (LEAT)
September 2010

 VYURA WA KIHANSI?
Hawa ni vyura wa ajabu! Wanapatikana katika maporomoko ya maji ya Kihansi na Muhalala, kusini mwa milima ya Udzungwa nchini Tanzania.
Vyura hawa ambao kwa jina la kitaalamu hujulikana kama ‘Nectophrynoides asperginis wanatajwa na wanasayansi kuwa miongoni mwa viumbe vilivyo katika hatari ya kutoweka kabisa kutokana na kuishi kweye makazi hatarishi, au kupoteza makazi yao ya asili na kupungua kwa idadi yao.
Vyura wa Kihansi waligunduliwa mnamo mwaka 1996 na timu iliyojumuisha wataalamu cha Elimu ya wanyama na Uhifadhi wa Wanyamapori kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika mchakato wa kufanya Tathmini ya athari za mazingira (Environmental Impact Assessment) kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa bwawa la uzalishaji wa umeme wa Kihansi.Ingawa yalitolewa mapendekezo ya namna ya kuwalinda viumbe hawa, mnamo mwaka 1996 karibu asilimia 90 ya maji ya mto Kihansi yalibadilishwa uelekeo kwa alili ya uzalishaji wa umeme kitu kilichopelekea upungufu mkubwa wa maji katika bonde la Kihansi, ambayo ndio hasa makazi ya vyura hawa. Kwa lugha rahisi kabisa ni kwamba mradi wa umeme uliyaharibu vibaya kama sio kutaka kuyapoteza makazi ya Maliasili hii ya kipekee.
Muathirika wa Kihansi
Mabadiliko haya yalikuwa na athari kubwa! Zaidi ya makazi ya viumbe hawa kuharibiwa, inaaminika kuwa kulikuwa na upungufu mkubwa wa hewa ya oksijeni ambayo ni muhimu sana kwa uhai wa viumbe wote, vilevile inaripotiwa kwamba kulikuwa na mlipuko wa ugonjwa wa ‘fangas’ walioenezwa viatu (mabuti) na Wahifadhi wa Mazigira pamoja na wataalamu katika kipindi cha utafiti. Kikubwa kuliko yote hakukuwa tena na uwiano wa kimazingira katika makazi hayo. Yote haya yalipelekea kupungua kwa vyura wa Kihansi kwa idadi inayokadiriwa kutoka vyura 50,000 hadi 12,000. Zaidi ya hapo ugonjwa wa fangas uliendelea kuua viumbe hawa kwa kasi kubwa.

Bonde la Kihansi kabla ya ujenzi wa mradi wa Umeme.

BWAWA LA UMEME LA KIHANSI
“Kwa wanamazingira na watetezi wa haki za wanyamapori, huu ulikuwa ni msiba mkubwa kushuhudia viumbe hawa wakitoweka kabisa. Kwao Umuhimu wa mradi wa umeme kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania usingetosha kama sababu ya kutokomeza vyura hawa. Kwa thamani ya mazingira mradi wa umeme unapaswa kutekelezwa kwa kuzingatia uhifadhi wa mazingira na viumbe waliomo, hivyo basi endapo mradi kama huu utatishia uhifadhi na usalama wa mazingira na viumbe itakuwa ni sababu ya msingi ya kupinga utekelezwaji wa mradi huo

UKOMBOZI WA KIMAZINGIRA
Bronx Zoo
Ilikuwa ni mwishoni mwa mwaka 2000 ambapo kilio cha wanamazingira kilisikika kikichagangiwa na msukumo wa taasisi za kimataifa pamoja muitikio chanya wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, donia ilishuhudia serikali ya Tanzania ikishirikiana na Jamii ya Uhifadhi wa Wanyamapori (‘the Wildlife Conservation Society-WCS)  ikisafirisha vyura 500 kutoka kwenye bonde la Kihansi,Tanzania kwa ndege maalumu kwenda nchini Marekani katika hifadhi ya Bronx (Bronx Zoo) na baadae kwenye hifadhi ya Taledo (Taledo Zoo) lengo likiwa kuwanusuru vyura hao wasipotee kwa kuwaweka katika mazingira yaliyo na hali karibu sawa na ile ya bonde la Kihansi kabla ya kuharibiwa na utekelezaji wa mradi wa umeme. Gharama iliyotumika kukamilisha zoezi la uhamishwaji wa vyura hawa pamoja na uhafadhi wake huko Marekani, hakika linatoa picha ya thamani ya uwepo wa kila kiumbe hapa duniani, kwani ni jambo lisilothibitika kuwa uwepo wa viumbe, akiwemo binadamu, unategemeana sana.
Baadhi ya Vyura waliorejea Tanzania.
Mwaka 2009 Muungano wa Kimataifa kwa Uhifadhi wa Asili - International Union for the Conservation of Nature (IUCN) ilitangaza rasmi kuwa vyura wa Kihansi kuwa miongoni mwa viumbe vilivyo katika hatari ya kutoweka duniani na hivyo kutoa wito kwa jamii ya kimataifa na wanaharakati wa mazingira duniani kwalinda Vyura hawa ambao ni maliasili adimu duniani. Hata hivyo kumekuwepo na faraja juu ya maisha ya vyura hawa katika kipindi cha maisha yao huko ugeninii. Hii inatokana na repoti kuwa idadi ya vyura hao imeongezeka inayokadiriwa kufikia vyura 7,000 kwa sasa.

KARIBU NYUMBANI VYURA WA KIHANSI.