Saturday, May 21, 2016

KIKUNDI CHA UFUGAJI NYUKI CHA KIJIJI CHA IHEFU WILAYA YA MUFINDI WAHITIMU MAFUNZO

Timu ya watu 22 wa kikundi cha ufugaji nyuki katika kijiji cha Ihefu wilayani Mufindi, wahitimu mafunzo ya siku tatu ya ufugaji nyuki.
Mafunzo hayo ambayo hutolewa na Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo(LEAT) yanalenga kuwezesha wananchi kuanzisha shughuli mbadala za kuongezea kipato katika vijiji 32 vinavyotekeleza mradi wa 'Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili' ...unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID). 

 Katika awamu ya kwanza ya mafunzo ya ufugaji nyuki wanakikundi walijifunza umuhimu wa asali kwa matumizi ya kila siku, aina za nyuki, ufugaji bora, jinsi ya kutundika mizinga na uvunaji bora.

Awamu ya pili ya mafunzo itahusu usindikaji na jinsi ya kutafuta masoko ndani na nje ya nchi.
Baada ya kuhitimu mafunzo kila mshiriki alipewa vitendea kazi ambavyo ni mzinga wa nyuki, nta, patasi na vifaa vya kujikinga na nyuki- kofia, wavu wa kuzuia uso, glavu, suti na viatu maalum.
Mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili unatekelezwa katika vijiji 32 vya wilaya za Iringa na Mufindi katika mkoa wa Iringa.

 Wilaya hizo zilichaguliwa kwasababu zina maeneo ya usimamizi wa wanyamapori, rasilimali za wanyamapori, misitu na maeneo ya hifadhi. Lengo kuu la mradi ni kuhakikisha kuwa wananchi wanashiriki kikamilifu katika usimamizi wa maliasili.
Pia kutetea usimamizi bora wa maliasili ilikupunguza umasikini na kuhakikisha uhifadhi endelevu wa uhainuai, kuiwezesha jamii kuwa na utamaduni wa ushiriki katika masuala yanayohusu maliasili, kuzijengea uwezo jamii za wenyeji uwezo wa katika kuziwajibisha na kuzisimamia taasisi za serikali zenye majukumu ya kuhifadhi na kusimamia maliasili.
Sehemu ya wanakikundi cha ufugaji nyuki wakiwa darasani


Baadhi ya wanakikundi cha ufugaji nyuki wakiwa katika mavazi ya kujikinga na nyuki

Wanakikundi cha ufugaji nyuki wakifuatilia mafunzo
 
 

Friday, May 13, 2016

MAFUNZO YA USIMAMIZI WA MALIASILI KATIKA KIJIJI CHA KINYIKA-WILAYA YA IRINGA

Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) kwa kushirikiana na Asasi ya MBOMIPA ambao ni watekelezaji wenza katika mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili, wamehitimisha mafunzo ya siku saba katika kijiji cha Kinyika, wilaya ya Iringa.

 Kijiji cha kinyika ni moja ya vijiji vilivyopo katika eneo la Usimamizi wa Wanyamapori linalosimamiwa na Asasi ya MBOMIPA, hivyo mafunzo hayo ni muhimu katika kuhakikisha kuwa wananchi wa maeneo hayo; wanafahamu haki yao ya kikatiba katika kusimamia rasilimali misitu na wanyamapori kwa maendeleo endelevu ya kizazi cha sasa na kijacho.

 Hapa nchini na maeneo mengine duniani, kumezuka wimbi la watu wachache kuvuna rasilimali misitu na wanayamapori kwa manufaa binfsi ambayo si rafiki kiuchumi na kimazingira. Tumeshuhudia wanyapori wakiuawa kwa kasi sana na hasa tembo, simba na chui.

Pia katika sekta ya misitu tumeshuhudia uvunaji haramu na usio endelevu unao hatarisha hatma ya kizazi hiki.
Mafunzo hayo yalihusu mambo muhimu katika usimamizi dumivu wa misitu na wanyamapori, kwa kuangalia sera na sheria zinasema nini katika kusimamia rasilimali hizo. Pia, washiriki waliangalia miongozo, kanuni na adhabu, ambazo zitawasaidia katika kutengeneza sheria ndogondogo za vijiji za usimamizi wa maliasili.

Mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili umefadhiliwa na Watu wa Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID). Mradi unatekelezwa katika vijiji 32 vya wilaya za Iringa na Mufindi, mkoani Iringa.
Baadhi ya Washiriki wa mafunzo wakijibu maswali ya awali kabla ya mafunzo, ilikupima wanaelewa kiasigani dhana ya Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa maliasili
 
 
 
Washiriki wa mafunzo katika kazi za vikundi
 
Afisa Ugani wa LEAT, Hana Lupembe (aliye vaa gauni jekundu) katika piacha ya pamoja na Washiriki wa mafunzo

WANANCHI WA VIJIJI VYA IFWAGI NA LUDILO WANOLEWA

Wananchi wa vijiji vya Ifwagi na Ludilo katika Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa wahudhuria mafunzo ya siku saba yaliyotolewa na Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo' (LEAT) kwa kushirikiana na Asasi ya Kiraia ya ASH-TECH ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa 'Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili', unaofadhiliwa na Watu wa Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID).

Kwa mujibu wa Afisa Ugani wa LEAT kwa wilaya ya Mufindi, Franklyn Masikia, takribani wananchi 120 walihudhuria mafunzo hayo, ambayo yalihusu Usimamizi wa Maliasili na Ufuatiliaji Uwajibikaji Jamii.
Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wananchi kushiriki kikamilifu katika usimamizi wa rasiliami misitu na wanyamapori, ilikuzinusuru na hatari ya kutoweka kutokana na kukithiri kwa uvunaji usio endelevu.

 Pia kupitia mafunzo ya Ufuatiliaji Uwajibikaji Jamii, wananchi watakuwa na uwezo wa kuwa wajibisha viongozi wao kwa kudai uwazi katika kupanga matumizi ya maliasili, sambamba na kuhoji mapato na matumizi yatokanayo na rasilimali zinazopatikana katika vijiji vyao.
Mafunzo hayo yalianza mwanzoni mwa mwezi Mei, katika nyakati tofauti, ambapo kila kijiji kilikuwa na washiriki 60.

Katika mafunzo hayo, wananchi walipata fursa ya kuzifahamu sera, sheria na miongozo katika usimamizi dumivu wa maliasili. Pia, Washiriki waliweza kuona wajibu na umuhimu wa wadau mbalimbali katika sekta ya maliasili, ikiwemo taasisi zinazo simamia, mashirika ya kijamii ya kitaifa na kimataifa, wizara, pamioja na wajibu wa wananchi katika usimamizi wa maliasili.

  Mradi huu unatekelezwa katika vijiji 32 vya wilaya za Iringa vijijini na Mufindi, mkoani Iringa. Takriban wananchi 6500 watafikiwa na mradi huu.

Sehemu ya Washiriki wa mafunzo katika kijiji cha Ludilo wakimsikiliza Mwezeshaji kutoka Asasi ya ASH-TECH, Thomas Mtelega
Katika picha ya pamoja na Washiriki wa mafunzo kijiji cha Ifwagi

Wednesday, May 11, 2016

WANANCHI WA KIJIJI CHA MWITIKILWA WAJIPANGA UFUGAJI NYUKI


 Kikundi cha wafugaji nyuki cha kijiji cha Mwitikilwa cha wilaya ya Mufindi chajipanga kuzalisha asali kwa wingi ilikukidhi mahitaji katika jamii.
Kikundi hicho cha watu 22 kilihudhuria mafunzo ya siku tatu mahususi kwa ufugaji bora na wenye tija. Baada ya mafunzo kikundi kilipatiwa vitendea kazi, vikiwemo suti, glavu, kofia, wavu wa kujikinga uso, viatu, patasi na nta.

 Mafunzo ya ufugaji nyuki ni sehemeu ya utekelezaji wa mradi wa 'Ushiriki wa Wananachi katika Usimamizi wa Maliasili' mradi unaotekelezwa na Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) kwa ufadhili wa watu wa Marekani, kupitia shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID). Mradi unatekelezwa katika vijiji 32 vya wilaya mbili za mkoa wa Iringa, wilaya ya Mufindi na Iringa.

 Lengo la mafunzo ya ufugaji nyuki ni kusaidia jamii zinazoishi karibu na rasilimali misitu na wanyamapori, kuinua uchumi wao bila ya kutegemea zaidi katika rasilimali zinazo wazunguka. Rasilimali ambazo ni chache na zinazo hitaji kutunzwa vizuri kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo.

Mafunzo haya yalitolewa na Afisa Nyuki wa wilaya ya Mufindi, Hamis Hassan, na Thomas Mtelega wa Asasi ya ASH-TECH ambao ni washiriki wa utelekezaji wa mradi.

Wanakikundi cha ufugaji nyuki wakifuatilia mafunzo kutoka kwa Afisa Nyuki wa Wilaya ya Mufindi bwana Hamis Hassan (Hayupo pichani)


Baadhi ya wanakikundi cha ufugaji nyuki wakiwa na Afisa Nyuki wa Wilaya ya Mufindi bwana Hamis Hassan (wa kwanza kushoto mstari wa mbele-mwenye koti la bluu bahari bila kofia)

 

MAANDALIZI YA UFUGAJI NYUKI YAKAMALIKA KATIKA KIJIJI CHA LUDILO-WILAYA YA MUFINDI


 Tarehe 8 Mei 2016, Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) iligawa mizinga 22 kwa kikundi cha wafugaji nyuki 22 wa kijiji cha Ludilo, wilayani Mufindi katika mkoa wa Iringa.
Wanakikundi pia walipatiwa nyenzo muhimu iliwaweze kutekeleza kazi hiyo kwa ufanisi. Nyenzo hizo ni pamoja na suti maalum, kofia, wavu wa kujikinga usoni, glavu, viatu, patasi na nta.

Kabla ya kugawiwa mizinga kikundi kilipatiwa mafunzo ya siku tatu ya ufugaji nyuki ambapo walijifunza namna bora ya ufugaji nyuki, aina za nyuki na umuhimu wa asali kwa matumizi ya kila siku. Pia, kikundi kitapatiwa mafunzo ya namna ya kufungasha asali na utafutaji masoko.

 Kutokana na umihumu wa asali kwa matumizi ya kila siku, kumekuwa na mwamko mkubwa wa watu kutumia asali, hali hiyo inatoa fursa za ajira kwa wakazi wa maeneo yanayofuga nyuki.

Mradi wa ufugaji nyuki ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili, unaotekelezwa na Timu wa Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) na kufadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID).

Moja ya lengo la mradi ni kuhakikisha kuwa Wananchi wanaoishi katika maeneo yenye rasilimali misitu na wanyamapori wanashiriki kikamilifu kuhifadhi na kulinda maliasili hizo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Ilikufikia lengo hilo, mradi wa ufugaji nyuki ni moja ya njia zitakazo wasaidia wananchi kupata vipato bila ya kutegemea rasilimali misitu, na wanyamapori; ilikuwa na mpango dumivu wa rasilimali hizo.
Afisa akisaidia kumvalisha glavu mmoja wa wanakikundi cha kufuga nyuki

Kikundi cha ufugaji nyuki katika mavazi rasmi ya kujikinga na nyuki mbele ya wananchi wa kijiji cha Ludilo

 

TUNASONGA MBELE-MAFUNZO YA UFUGAJI NYUKI IFWAGI-Wilaya ya Mufindi-Iringa


 MAFUNZO YA UFUGAJI NYUKI IFWAGI-Wilaya ya Mufindi, Iringa
Kikundi cha ufugaji nyuki cha watu 22 cha kijiji cha Ifwagi, wilaya ya Mufundi chapatiwa mafunzo ya ufugaji nyuki kwa siku tatu, pamoja na mizinga 22 ya kufugia, na vifaa vya kujikinga na nyuki ambavyo ni kofia, wavu wa kujikinga usoni, glavu, na viatu maalumu. Pia walipatiwa  patasi na nta.

 Baada ya mafunzo wanakikundi cha ufugaji nyuki, Afisa Nyuki wa wilaya ya Mufindi, mwakilishi wa Asasi ya ASH-TECH pamoja na Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazinigira kwa vitendo(LEAT), walitembelea msitu wa asili wa Kidege ili kuainisha eneo litakalo tundikwa mizinga ya nyuki.

 Mafunzo ya ufugaji nyuki yanawapatia wakazi wa kijiji cha Ifwagi chanzo mbadala cha mapato, ilikupunguza utegemezi wa mapato yatokanayo na rasilimali za msitu wa asili wa kidege. Msitu wa asili wa Kidege unategemewa na vijiji vitatu ambavyo ni Ifwagi, Mwitikilwa na Ludilo.


Mradi wa ufugaji nyuki utasaidia kupunguza utegemezi wa mapato unaotokana na rasilimali misitu na wanyamapori katika vijiji ambavyo vinatekeleza mradi wa 'Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili', unaotekelezwa na LEAT katika vijiji 32 vya wilaya za Iringa na Mufindi, mkoani Iringa.

 
 Mradi wa Ushiriki wa Wananachi katika Usimamizi wa Maliasili unafadhiliwa na Watu wa Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID), ulianza Novemba 2014 na unatarajiwa kukamilika Novemba 2017.

Baadhi ya Wanakikundi wakiwaonesha wenzao namna ya kutundika mzinga wa nyuki baada ya mafunzo. Aliyevaa koti jeusi ni Afisa Nyuki wa Wilaya ya Mufindi bwana Hamis Hassan.
 
Wanakikundi wakifuatilia mafunzo
Wanakikundi wakiwa na Afisa Nyuki wa Wilaya ya Mufindi, Hamis Hassan (wa pili kushoto) Boksi jeupe linalo ning'inia kwenye mti ni moja ya mizinga iliyogawiwa na LEAT kwa kikundi hicho.
 
.

 

Saturday, May 7, 2016

VIKUNDI VYA UFUGAJI NYUKI VYAPATIWA VITENDEA KAZI

Vikundi vya ufugaji nyuki katika vijiji vya Malinzanga, Kiwere, Mfyome, Kitapilimwa, Itagutwa, Kitisi na Idodi. Kila kijiji kina kikundi kimoja chenye watu 22. Baada ya kupatiwa mafunzo ya ufugaji nyuki kila mwanakikundi alipatiwa mzinga wa kufugia nyuki, na awamu ya pili walipatiwa vifaa vya ufugaji nyuki ikiwa ni pamoja na kofia, nyavu, glavu, suti na viatu maalumu vya kujikinga na nyuki. Zifuatazo ni picha za ugawaji wa vitendea kazi hivyo.
Afisa Vifaa bwana Mremi akiteremsha vifaa vya ufugaji nyuki tayari kwa kuwagawia wanakikundi cha ufugaji nyuki wa kijiji cha Idodi, wilayani Iringa

 
Wa pili kushoto afisa Ugani, Hana Lupembe akiwa pamoja na wanakikundi cha ufugaji nyuki wa kijiji cha Idodi. Mmoja wa wanakikundi akiwa amevalia mavazi rasmi ya ufugaji nyuki
 
Afisa Vifaa bwana Mremi akisaidia kumvalisha mavazi ya kujikinga na nyuki, mmoja wa wanakikundi cha ufugaji nyuki wa kijiji cha Kitisi

Afisa Ugani Hana Lupembe akimkabidhi Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kitisi, vifaa vya kujikinga na nyuki kwaajili ya wanakikundi wa ufugaji nyuki. Wanao shuhudia ni baadhi ya wanakikundi cha ufugaju nyuki

Mwenyekiti wa Asasi ya MJUMIKK ambao ni wadau wa utekelezaji wa maradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili, Mashaka Kilanga, akimuelekeza mmoja wa wanakikundi cha ufugaji nyuki jinsi ya kuvaa mavazi ya kujikinga na nyuki katika kijiji cha Itagutwa, wilaya ya Iringa
 
KIJIJI CHA KITAPILIMWA-TENDA KAMA MWENYE MALI!
Afisa Ugani Hana Lupembe akiwa anatafuta mtandao wa simu kwaajili ya kuwasiliana na Makao Makuu Dar es Salaam. Ilimlazimu apande juu ya mti kutafuta mawasilino.
 

Kutoka kulia: Afisa Ugani Hana Lupembe na bwana Komba (mwenye nguo nyeusi) wakiwa na baadhi ya wanakikundi cha ufugaji nyuki kijijini Kitapilimwa
 
 
(Wa tatu kushoto)Mwenyekiti bwana Kilanga na (wa pili kushoto)Mratibu bwana Komba wa Asasi ya MJUMIKK, wakipata maelezo kutoka kwa kikundi cha ufugaji nyuki, walipo tembelea enao la kufugia nyuki kijijini Kitapilimwa

Afisa Ugani, Hana Lupembe akisoma orodha ya vifaa vya kujikinga na nyuki alivyokabidhi kwa kikundi cha ufugaji nyuki- Mfyome


Mwanakikundi cha ufugaji nyuki akiwa katika mavazi ya kujikinga na nyuki katika eneo la kufugia nyuki- Mfyome


Afisa Ugani, Hana Lupembe akikagua mizinga iliyotundikwa katika eneo la kufugia nyuki katika kijiji cah Kiwere, wilaya ya Iringa
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kiwere (mwenye koti jeusi) alipewa heshima na LEAT ya kugawa vifaa vya kujikinga na nyuki kwa wanakikundi cha ufugaji nyuki-Kiwere

Katika picha ya pamoja: Kutoka kulia waliokaa: Afisa Mtendaji wa kijiji cha Kiwere, Mratibu wa Asasi ya MJUMIKK, Mwenyekiti wa Asasi ya MJUMIKK na mwanakikundi cha ufugaji nyuki.
Waliosimama kutoka kulia: Afisa Ugani Hana Lupembe akiwa na baadhi ya wanakikundi cha ufugaji nyuki, baada ya kugawiwa mavazi ya kujikinga na nyuki.


Mwanakikundi cha ufugaji nyuki wa kijiji cha Malinzanga akivaa mavazi ya kujikinga na nyuki, mara baada ya kugawiwa na LEAT.
Kuelekea eneo la ufugaji nyuki- Iliwalazimu kuacha gari mbali kigodo- Afisa Vifaa bwana Mremi akivuka mto kuelekea eneo la kufugia nyuki-Malinzanga
Eneo la kufugia nyuki Malinzanga-Wanakikundiwakionesha mizinga waliyotundika

LEAT YAGAWA VIFAA VYA UFUGAJI NYUKI


Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa vitendo (LEAT) imegawa vifaa vya ufugaji nyuki katika vijiji ambayo vinatekeleza mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili, unaofadhiliwa na Watu wa Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID). Mradi huu unatelekezwa katika vijiji 32 vya wilaya za Iringa na Mufindi, mkoani Iringa.

Mradi wa ufugaji nyuki unalenga kusaidia jamii zilizozungukwa na rasilimali misitu na wanyamapori, kujipatia kipato mbadala ilikupunguza utegemezi wa kipato unaotokana na maliasili zilizo wazunguka.

Mradi wa ufugaji nyuki umelenga kuwafikia wananchi 700, kwa kupatiwa mafunzo ya ufugaji nyuki pamoja na kupewa mizinga na vifaa vya ufugaji nyuki. Kila mwananchi aliyepatiwa mafunzo hayo, hupewa mzinga mmoja na vifaa, ikiwemo kofia, wavu wa kuzuia kuumwa na nyuki, suti, glavu na viatu maalum.

Vifaa vya ufugaji nyuki na mizinga hugawiwa kwa awamu tofauti, kwa awamu hii jumla ya vijiji nane vimefikiwa. Vijiji hivyo ni Malinzanga, Kiwere,Mfyome, Kitapilimwa, Itagutwa, Tungamalenga, Kitisi na Idodi.

Afisa Ugani wa LEAT Hna Lupemba (kulia) akigawa vifaa vya uafugaji nyuki kwa wanakikundi wa kijiji cha Tungamalenga, wilayani Iringa

Mmoja wa wanakikundi caha ufugaji nyuki wa Tungamalenga akisaidia kumvalisha mwenyekiti wa kijiji
Mwenyekiti wa kijiji cha Tungamalenga akiwa katika mavazi ya ufugaji nyuki
Baadhi ya vifaa vya ufugaji nyuki vilivyo gawiwa kwa wanakikukndi, kijijini Tungamalenga

Friday, May 6, 2016

Yaliyojiri katika Mkutano wa Tathmini ya nusu mwaka ya Mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili


Wadau wa Mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili Waipongeza LEAT

Wadau wa mradi wa Ushiriki wa wananchi katika Usimamizi wa Maliasili waipongeza Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo, kwa kutekeleza shughuli za mradi kwa kushirikisha wadau wote muhimu.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa alisema haya………

Akiongea wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tathmini ya maendeleo ya mradi kwa kipindi cha miezi sita, kuanzia Novemba 2015 hadi Aprili 2016, Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mheshimiwa Richard Kasesela, alisema taasisi ya LEAT imefanikiwa katika utekelezaji za mradi wake kwasababu ya utaratibu mzuri waliojiwekea, ikiwemo kushirikisha wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Ofisi za Wakuu wa Wilaya, Halmashauri za Wilaya, Serikali za vijiji, Mashirika ya kijamii, wananchi pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.
Kutoka kushoto: Mkurugenzi Mtendaji wa LEAT, Dkt. Rugemeleza Nshala na Mkuu wa wilaya ya Iringa, Mh. Richard Kasesela

Alisema’ LEAT imepokelewa vizuri na wananchi wa Iringa kwasababu walitambua umuhimu wa kushirikisha wadau wote toka kuanza kwa mradi hivyo wananchi wanauthamini mradi na kuona kuwa wao ni sehemu ya mafanikio ya mradi’.

Alifafanua kuwa mafaniko ya mradi wa LEAT ni pamoja na mwitikio mkubwa wa wananchi kushiriki katika usimamizi wa maliasili, kwa kutoa taarifa za uhujumu maliasili unaoendana sambamba na ukamataji wa rasilimali za misitu.

Mkuu wa Wilaya alitolea mfano, wananchi walivyoweza kukamata mbao 298 mwezi Januari 2016, katika kijiji cha Mfyome, na mbao 491 zilizokamatwa katika kijiji cha Tungamalenga wilayani Iringa.

Pia alipendekeza LEAT na waandishi wa habari waanzishe ukurasa katika mitandao ya kijamii kwaajili ya kuwaripoti waharibifu wa mazingira, ikiwa ni Pamoja na kuweka picha zao katika kurasa hizo. Alisema kutokana na kasi kubwa ya uvunaji miti, ipo haja ya wadau wote kuanzisha kampeni ya kutokomeza uvunaji haramu kama inavyofanyika kampeni ya kuzuia mauaji ya tembo.
 

 
Kutoka ushoto: Mwenyekiti wa Halmashauri Mufindi, Ashery Mtono, Mkurugenzi Mtendaji wa LEAT, Dkt. Rugemeleza Nshala na Mkuu wa Wilya ya Iringa, Richard Kasesela

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iringa Alonga…..

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Hamlashauri ya Iringa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Halmashauri za Iringa, Mheshimiwa Steven Mhapa alisema kuwa miradi mingi iliyotekelezwa mkoani Iringa haikuweza kuendelezwa kwasababu serikali na wananchi hawakushirikishwa kikamilifu kuanzia katika hatua za awali za mradi, hivyo wadau hao huhisi kuwa wao sio muhimu katika kufikia malengo ya mradi.

Aliye simama ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iringa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Mkoa wa Iringa, Mh. Steven Mhapa

 “Nawapongeza LEAT kwakuwa wanafahamu umuhimu wa wadau wote katika kufikia malengo ya mradi, walishirikisha ofisi ya Wakuu wa Wilaya, Halmashauri na wananchi, ndio maana hata leo hii tumejumuika nao katika mkutano wa tathmini ya mradi, kwa kuwa na sisi ni sehemeu ya mafanikio ya mradi.

Mheshimiwa Mhapa alitoa angalizo kuwa kutokana na umuhimu wa maliasili katika ustawi wa uchumi wa nchi,LEAT iangalie namna itakavyoweza kuongeza wigo wa mradi katika wilaya nyingine za mkoa wa Iringa, ili wananchi waliozungukwa na maliasili wafahamu thamani ya rasilimali misitu hususan mbao. Alisema serilkali za vijiji vinvyozungukwa na rasilimali misitu zinapokea mapato hafifu ambayo hayalingani na thamani ya miti inayovunwa.

Tutaendelea kushirikiana na LEAT-Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mufindi                                                                                                            

Mheshimiwa Ashery Mtono, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mufindi alisema kuwa halmashauri yake itaendelea kushirikiana na LEAT kwakuwa wameona mafanikio ya mradi katika halmashauri yake. Alisema wananchi wamepata mwamko mkubwa kuhusu ushiriki waa katika usimamizi wa maliasili, kuwa matukio ya ukamataji wahujumu maliasili yameongezeka, pia wananchi wamepata ujasiri wa kuhoji viongozi wao juu ya mapato na matumizi ya maliasili. Pia wananchi wana ujasiri wa kudai uwazi na uwajibikaji kutoka kwa viongozi wao, hivyo kuboresha utoaji wa huduma za jamii.
Aliyesimama: Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mufindi, Mh. Ashery Mtono

Mkurugenzi Mtendaji wa LEAT aelezea lengo la mkutano wa tathmini ya mradi                                                                                                  

Akizungumza katika mkutano wa tathmini ya mradi kwa kipindi cha miezi sita, Novemba 2015 hadi Aprili 2016, Mkurugenzi Mtendaji wa Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT), Dkt. Rugemeleza Nshala alisema kuwa lengo la mkutano ilikuwa kupima utekelezaji wa mradi, kwa kuangalia mafanikio, changamoto na mipango ijayo ilikuhakikisha kuwa wadau wote kila mmoja kwa nafasi yake anashiriki kikamilifu ilikufikia malengo ya mradi.

Mkurugenzi Mtendaji wa LEAT, Dkt. Rugemeleza Nshala akiwasilisha taarifa ya jumla ya maendeleo ya mradi
Afisa Mradi Mwandamizi, Remmy Lema, akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya mradi
Timu ya LEAT: Kutoka kushoto: Hadija Mrisho, Glory Kilawe, Edina Tibaijuka na Glory Ephraem
 
Pia aliwashukuru viongozi wa Wilaya na Halmashauri za Iringa na Mufindi kwa kushiriki bila kuchoka tangu kuanza kwa mradi mwaka 2014 mpaka sasa.Pia aliwajulisha wadau kuwa milango ya LEAT ipo wazi ilikutoa fursa kwa wadau wote kutoa mchango ya kuboresha utekelezaji wa mradi.

LEAT imeboresha utendaji wake -Mwakilishi kutoka Chemonics         

Mwakilishi kutoka shirika la Chemonics, Thobias Chelechele, ambao ni Wakala wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID-Wafadhili wa mradi), aliipongeza LEAT kwa kuboresha utendaji wake, na kuwa hiyo ni kiashiria cha kufanikiwa kwa mradi.
Kutoka kushoto: Afisa Mradi Mwandamizi wa LEAT, Remmy Lema na Mwakilishi wa Chemonics Tanzania, Thobias Chelechele

Bwana Thobia,pia alizishauri Asasi za kiraia kuhakikisha kuwa wanafuata miongozo ya uendeshaji shirika ikiwemo masuala ya utawala, fedha, utunzaji kumbukumbu na utekelezaji mradi kwa ujumla, iliwaweze kukua na kujiweka katika nafasi nzuri ya kupata fedha baada ya mradi huu kwisha.                                                   

Mkutano huo ulihudhuriwa na wadau kutoka wilaya za Iringa na Mufindi, akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Wenyeviti wa halmashauri, Wakuu wa idara za maliasili, Waruzuku wa mradi, asasi za kiraia na wananchi.

Mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili unatekelezwa katika wilaya za Iringa na Mufindi, mkoani Iringa. Mradi huu umefadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID), na unatekelezwa na Timua ya Wanansheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) kwa kushirikiana na Asasi za Kiraia.

Asasi za Kiraia wapatiwa Vitendea Kazi

Asasi za Kiraia ambazo pia ni watekelezaji wa mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili, wapatiwa kompyuta mpakato (laptop) ilikurahisisha utendaji wa shuguli zao. Asasi za Kiraia zilizopokea kompyuta mpakato ni MBOMIPA, MUVIMA, ASH-TECH na MJUMIKK.

 

 

 
 
 
Mkurugenzi wa Asasi ya kiraia ya ASH-TECH, Erasto Mazera akipokea kopmyuta mpakato kwaajili ya kurahisisha utekelezaji wa mradi
 
 

Mwenyekiti wa MBOMIP akipokea kompyuta mpakato
Mwenyekiti wa Asasi ya MJUMIKK, Mashaka Kilanga akipokea kompyuta mpakato


Mkurugenzi wa MUVIMA akipoke kompyuta mpakato
 
Bwana Komba akiwasilisha sehemu ya utekelezaji ya asasi yake ya MJUMIKK
Sehemu ya Wadau wakifuatilia mawasilisho kutoka kwa watekelezaji mbalimbali wa mradi
 
Wadau wa mradi wakifuatilia mawasilisho ya maendeleo ya maradi