Wednesday, February 3, 2016

HATARI-HATUNA NJIA MBADALA YA MAJI TAKA-WALIMA MBOGAMBOGA WASEMA

 
Wakulima wa mbogamboga jijini Dar Es Salaam wamesema kuwa hawana njia mbadala ya kutumia maji taka kumwagilia bustani zao kwakuwa hawapati maji safi kwaajili ya umwagiliaji.
Wakulima waliyasema hayo wakati wa mahojiano na mwandishi wa gazeti la The Guradian, tarehe 02/02/2016. Walisema kuwa wame elekeza katika bustani zao mifereji inayo tiririsha majitaka kutoka katika makazi ya watu. Walisisitiza kuwa iwapo maji safi kutoka katika mabomba au visima yangekuwa yanapatikana kwa urahisi wangetumia hayo badala ya kutumia maji taka.
 
Tarehe 02/02/2016 gazeti la The Guradian lilishapisha katika ukurasa wake wa mbele kuwa Mamlaka ya Uthibiti Anfya nchini imeonya kuwa watu waishio katika  majiji na mijini wanao kula mboga zinazolimwa katika bustani za mijini wapo katika hatari ya kiafya ikiwemo kupata maradhi yasiyo tibika.
 
Wakitoa angalizo hilo kwa Pamoja Mamlaka ya Chakula na Dawa na Taasisi ya Chakula na Lishe walisema matumiza ya maji taka kwenye mazao ya mboga za majani na matunda, kachumbari na matunda huwa na bakteria ambao huingia katika tumbo la binadamu na kusababisha magonjwa kama vile saratani, ugonjwa wa figo na kuathiri mfumo wa fahamu kwa watoto.
 
Kwa mujibu wa bwana Edward Melkion ambaye amekuwa akilima mboga za majani katika bonde Msimbazi tangu mwaka 1991, yeye Pamoja na wenzake wameelekza katika vitalu vyao mrefeji wa maji taka unaotirirsha maji kutoka Buguruni, kwa kisingizio cha kukosa maji safi kwaajili ya umwagiliaji.
 
 
Akitoa angalizo Mtafiti wa Mafunzo Lishe wa Taasisi ya Chakula na Lishe, bwana Walbert Mgeni alisema bakteria wanao patikana katika mboga za majani
 
hufa iwapo mboga zitapikwa kwa muda mrefu lakini kemikali kama vile madini ya chuma katika mboga hayapotei bali huingia mwilini.
 

Sehemu ya bustani zinazolimwa katika bonde la Msimbazi Dar Es Salaam

Sehemu ya bustani ya nyanya iliyopo katika eneo la bonde la Msimbazi, Dar Es Salaam
 
 
 
 
 
 
 
 

No comments:

Post a Comment