Saturday, May 7, 2016

VIKUNDI VYA UFUGAJI NYUKI VYAPATIWA VITENDEA KAZI

Vikundi vya ufugaji nyuki katika vijiji vya Malinzanga, Kiwere, Mfyome, Kitapilimwa, Itagutwa, Kitisi na Idodi. Kila kijiji kina kikundi kimoja chenye watu 22. Baada ya kupatiwa mafunzo ya ufugaji nyuki kila mwanakikundi alipatiwa mzinga wa kufugia nyuki, na awamu ya pili walipatiwa vifaa vya ufugaji nyuki ikiwa ni pamoja na kofia, nyavu, glavu, suti na viatu maalumu vya kujikinga na nyuki. Zifuatazo ni picha za ugawaji wa vitendea kazi hivyo.
Afisa Vifaa bwana Mremi akiteremsha vifaa vya ufugaji nyuki tayari kwa kuwagawia wanakikundi cha ufugaji nyuki wa kijiji cha Idodi, wilayani Iringa

 
Wa pili kushoto afisa Ugani, Hana Lupembe akiwa pamoja na wanakikundi cha ufugaji nyuki wa kijiji cha Idodi. Mmoja wa wanakikundi akiwa amevalia mavazi rasmi ya ufugaji nyuki
 
Afisa Vifaa bwana Mremi akisaidia kumvalisha mavazi ya kujikinga na nyuki, mmoja wa wanakikundi cha ufugaji nyuki wa kijiji cha Kitisi

Afisa Ugani Hana Lupembe akimkabidhi Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kitisi, vifaa vya kujikinga na nyuki kwaajili ya wanakikundi wa ufugaji nyuki. Wanao shuhudia ni baadhi ya wanakikundi cha ufugaju nyuki

Mwenyekiti wa Asasi ya MJUMIKK ambao ni wadau wa utekelezaji wa maradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili, Mashaka Kilanga, akimuelekeza mmoja wa wanakikundi cha ufugaji nyuki jinsi ya kuvaa mavazi ya kujikinga na nyuki katika kijiji cha Itagutwa, wilaya ya Iringa
 
KIJIJI CHA KITAPILIMWA-TENDA KAMA MWENYE MALI!
Afisa Ugani Hana Lupembe akiwa anatafuta mtandao wa simu kwaajili ya kuwasiliana na Makao Makuu Dar es Salaam. Ilimlazimu apande juu ya mti kutafuta mawasilino.
 

Kutoka kulia: Afisa Ugani Hana Lupembe na bwana Komba (mwenye nguo nyeusi) wakiwa na baadhi ya wanakikundi cha ufugaji nyuki kijijini Kitapilimwa
 
 
(Wa tatu kushoto)Mwenyekiti bwana Kilanga na (wa pili kushoto)Mratibu bwana Komba wa Asasi ya MJUMIKK, wakipata maelezo kutoka kwa kikundi cha ufugaji nyuki, walipo tembelea enao la kufugia nyuki kijijini Kitapilimwa

Afisa Ugani, Hana Lupembe akisoma orodha ya vifaa vya kujikinga na nyuki alivyokabidhi kwa kikundi cha ufugaji nyuki- Mfyome


Mwanakikundi cha ufugaji nyuki akiwa katika mavazi ya kujikinga na nyuki katika eneo la kufugia nyuki- Mfyome


Afisa Ugani, Hana Lupembe akikagua mizinga iliyotundikwa katika eneo la kufugia nyuki katika kijiji cah Kiwere, wilaya ya Iringa
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kiwere (mwenye koti jeusi) alipewa heshima na LEAT ya kugawa vifaa vya kujikinga na nyuki kwa wanakikundi cha ufugaji nyuki-Kiwere

Katika picha ya pamoja: Kutoka kulia waliokaa: Afisa Mtendaji wa kijiji cha Kiwere, Mratibu wa Asasi ya MJUMIKK, Mwenyekiti wa Asasi ya MJUMIKK na mwanakikundi cha ufugaji nyuki.
Waliosimama kutoka kulia: Afisa Ugani Hana Lupembe akiwa na baadhi ya wanakikundi cha ufugaji nyuki, baada ya kugawiwa mavazi ya kujikinga na nyuki.


Mwanakikundi cha ufugaji nyuki wa kijiji cha Malinzanga akivaa mavazi ya kujikinga na nyuki, mara baada ya kugawiwa na LEAT.
Kuelekea eneo la ufugaji nyuki- Iliwalazimu kuacha gari mbali kigodo- Afisa Vifaa bwana Mremi akivuka mto kuelekea eneo la kufugia nyuki-Malinzanga
Eneo la kufugia nyuki Malinzanga-Wanakikundiwakionesha mizinga waliyotundika

No comments:

Post a Comment