Saturday, June 3, 2017

PROF. ANNA TIBAIJUKA ATAMKA KUWA GHARAMA YA SERIKALI KUIPUUZA LEAT IMEONEKANA




Mkutano wa Saba wa Bunge umeendelea Dodoma. Kazi kubwa ikiwa ni mapendekezo ya wabunge katika bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini ambapo miongoni mwa waliopata nafasi ya kuchangia ni Mbunge wa Muleba Kusini Professor Anna Tibaijuka.

"Mhe Spika kuna Taasisi ya Lawyers' Environmental Action Team (LEAT) ina vijana wamekaa  vizuri sana. Sasa wamekuwa wakipuuzwa wakati wote na gharama ya kupuuzwa mnaiona". Alisema Prof. Anna Tibaijuka.

"Tuweke utamaduni wa kuwaheshimu na kuwasikiliza wataalam wetu. Tukiendelea kuwaita wanaharakati huku tukiwabeza na kuwapuuza, hatutatoka hapa tulipo". Aliongezea Prof. Tibaijuka


Tafadhali fungua video hiyo hapo juu kupata taarifa kwa kirefu.

No comments:

Post a Comment