Saturday, November 26, 2016

LEAT YATEMEBELEWA NA WATAALAM KUTOKA CHEMONICS INTERNATIONAL - USAID KWAAJILI YA KUREKODI VIDEO YA MAFANIKIO YA SHUGHULI ZA MRADI WA CEGO


 


Kutoka Kulia ni Bi. Karina Keating (Meneja mradi Pamoja Twajenga), Remmy Lema (Afisa Mradi Mwandamizi -LEAT), M/Kiti wa MJUMIKIK na Bw. Hamza Chang'a (Mwanilishi wa kikundi cha utunzaji wa mazingira kijiji cha Kiwere) Musa Mnasizu (Afisa Mradi wa CEGO wilaya ya Iringa), Dk. Rugemeleza Nshala (Mkurugenzi Mtendaji -LEAT) na wawili kushoto ni wajumbe wa kikundi cha Utunzaji wa mazingira-Kiwere wakionyesha kitalu cha miti walichokianzisha baada ya kupata mafunzo ya usimamizi wa maliasili kutoka LEAT


 
 
 
 Bw. Mike Bennett akichukua video ya mazungumzo kati ya Dk. Nshala Mkurugenzi Mtendaji wa LEAT na Bw. Hamza Chang'a akiwa na wajumbe wenzake wa kikundi cha Utunzaji wa mazingira, wakielezea faida ya mafunzo ya usimamizi wa maliasili kutoka LEAT iliyowasukuma kuanzisha kitalu cha miti.


 Bw. Mike Bennett Mwandishi kutoka Chemonics International-USAID akichukua video ya wanakijiji wa Kijiji cha Kiwere waliokuwa wakikata mti ulioanguka baada ya kuungua na moto.


Bwana Mike Bennett Mwandishi kutoka Chemonics International- USAID akipiga picha eneo la kijiji lililopandwa miti kutoka katika kitalu cha miti ya Kikundi cha Utunzanji mazingira cha kijiji cha Kiwere

 
 Afisa Ughani wa Mradi wa Ushiriki wa wananchi katika usimamizi wa maliasili (CEGO) wilaya ya Iringa akiwa na Bi. Karina Keating Meneja Mradi Chemonics International/Pamoja Twajenga katika ziara yao katika eneo lililopandwa miti na kikundi cha utunzaji mazingira katika ardhi ya kijiji cha Kiwere


Timu nzima ya mradi wa CEGO, Timu ya wataalamu kutoka Chemonics International-USAID na wanakikundi cha Utunzaji mazingira wa kijiji cha Kiwere wakizungukia eneo la ardhi ya kijiji lililopandwa miti na wanakikundi waliopatiwa mafunzo ya usimamizi wa maliasili kutoka LEAT kwa ufadhili wa USAID



 Kutoka Kushoto ni Bi. Karina Keating (Meneja-Pamoja Twajenga), Mike Bennett (Mwandishi-Chemonics International-USAID) , Dk. Rugemeleza Nshala (Murugenzi Mtendaji -LEAT) na Bi. Maria (Msimamizi wa miradi ya CEGO-Pamoja Twajenga) wakimrekodi Bw. Hamza Chan'ga aliyekuwa akielezea mafanikio ya elimu ya usimamizi wa maliasili kutoka LEAT Iliyowapelekea wanakijiji kuunda kikundi cha utunzaji wa mazingira na kuanzisha kitalu cha miti.



 
 





 Picha ya pamoja ya timu ya LEAT na wataalamu Kutoka Chemonics International baada ya kumaliza shughuli ya kurekodi simulizi za mafaniko zilizotokana na mradi wa ushiriki wa wananchi katika usimamizi wa maliasili (CEGO) unaotekelezwa na LEAT kupitia ufadhili wa shirika la maendeleo la Kimataifa la Marekani - USAID

 
Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID) linaloifadhili LEAT katika mradi wa ushiriki wa wananchi katika usimamizi wa maliasili (CEGO) walipendezwa na moja ya simulizi za mafaniko katika shughuli za mradi huu. Hivyo kutuma Afisa habari kutoka USAID-Chemonics International Ndugu Mike Bennett kuja kutembelea maeneo ya mradi yenye simulizi za mafanikio hayo. Mike Bennett aliongozana na Meneja Mradi  kutoka Pamoja Twajenga Bi. Karina Keating na Bi. Maria (Msimamizi wa asasi za miradi ya CEGO).

Timu hii ilitembelea kijiji cha Kiwere wilayani Iringa ambacho ni miongoni mwa vijiji vilivyopatiwa mafunzo ya Usimamizi wa maliasili, Ufuatiliaji wa uwajibikaji jamii (UJJ-SAM) na ufugaji nyuki yaliyowezeshwa na LEAT, Kijiji hiki kilionyesha matunda ya elimu waliyoipata kutoka LEAT kwa kuanzisha kikundi cha utunzanji wa mazingira huku lengo lao likiwa ni kutunza misitu inayoharibiwa kwa kasi kubwa katika maeneo yao.

 Miongoni mwa wanakijiji waliopatiwa mafunzo hayo katika kijiji cha Kiwere ni Bw. Hamza Hamis Chang’a  ambaye ni mwanzilishi na msimamizi wa shughuli za kikundi hiko. Bw. Hamza akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa LEAT na timu nzima ya mradi iliyotembelea kijiji hicho alisema, “kikundi hiki tulikianzisha baada ya kupata elimu nzuri ya usimamizi wa mazingira kutoka LEAT, tulipata muamko mkubwa wa kurejesha hali ya misitu yetu iliyoharibiwa kwa kiasi kikubwa, hivyo hatukutaka kuyalalia mafunzo hayo bali tulichukua jitihada za kuanzisha kikundi cha utunzanji wa mazingira kwa lengo la kutunza mazingira yaliyoharibiwa”

 Aliendelea “Jitihada zetu zilianza kwa kuanzisha kitalu cha miti. Tuliiomba halmshauri ya kijiji cha Kiwere itupatie eneo la wazi ili tupande miti hiyo. Kijiji kilitupatia eneo lenye ukubwa wa zaidi ya ekari mbili ambapo ndipo tulipopanda miti hiyo”.

Aliongezea Bwana Hamza kuwa “LEAT imetuhamasisha kwa kiasi kikubwa katika suala la utunzaji wa mazingira, na kupitia kikundi tulichoanzisha chenye takribani ya wajumbe 17 hadi sasa, tunaweza kuhifadhi misitu na kukuza kipato chetu kutokana na miche ya miti tutanayoiuza, kwani mpaka sasa tumeshauza miche kadhaa na kujipatia fedha kidogo iliyotusaidia kununua mbegu na kuotesha miche mingine kisha kiasi kilichobaki tuligawana kama faida kwa wanakikundi wote.

 

No comments:

Post a Comment