Sunday, November 27, 2016

LEAT YAIPA SERIKALI CHANGAMOTO YA MAZINGIRA KATIKA MDAHALO NA MKUTANO WA MAREJEO YA SHUGHULI ZA MRADI ULIOFANYIKA WILAYA YA IRINGA.

 Mkurugenzi Mtendaji wa LEAT Dk.Rugemeleza Nshala akifungua Mkutano wa marejeo wa Mradi wa CEGO na mdahalo uliowashirikisha viongozi wa serikali, wananchi na wadau wa maliasili mkoani Iringa.
 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza akihutubia na kufungua rasmi  Mkutano wa marejeo na Mdahalo uliotekelezwa na LEAT kupitia hisani ya watu wa Marekani -USAID
 Viongozi wa serikali ya wilaya ya Iringa na Mufindi wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa Bi. Amina Masenza na Muwakilishi kutoka USAID Bi. Joan Mayer.
 Timu ya Ufuatiliaji wa Uwajibikaji Jamii (UJJ/SAM) wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa serikali, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza (Katikati), Muwakilishi kutoka USAID Bi. Joan Mayer na Mkurugenzi Mtendaji wa LEAT Dk. Rugemeleza Nshala (Wa pili kulia)
 Timu ya utekelezaji wa mradi wa ushiriki wa wananchi katika usimamizi wa maliasili (CEGO) wilaya ya Iringa na Mufindi wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa serikali na Muwakilishi kutoka USAID Bi. Joan baada ya Mgeni Rasmi Bi Amina Masenza kufungua Mdahalo huo.

Mhadhiri Mwandamizi Chuo kikuu cha kilimo Morogoro (SUA) Dk. Gimbage Mbeyale akitoa mada ya kwanza kuhusiana na Chanzo cha kukithiri kwa changamoto mbalimbali katika usimamizi wa misitu na wanyamapori


Ndugu. Leo Mavita akitoa mada ya pili katika mdahalo kuhusiana na ni nini chanzo na athari za kutengwa kwa bajeti ndogo kwenye halmshauri za wilaya kwa ajili ya sekta ya misitu na wanyamapori.

Afisa Mradi Mwandamizi wa mradi wa ushiriki wa wananchi katika usimamizi wa maliasili (CEGO) Bw. Remmy Lema akitoa wasilisho la utukelezaji wa shughuli za mradi katika mkutano wa marejeo kwa wadau wa mradi na viongozi wa serikali mkoani Iringa.

 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mufindi Mh. Festo Mgina akizungumza katika mkutano wa marejeo na mdahalo uliofanywa na LEAT kwa hisani ya watu wa Marekani USAID



 Bw. Jeremiah Daffa - Mhamasishaji wa mdahalo na mkutano wa marejeo uliofanywa na LEAT kwa hisani ya watu wa Marekani (USAID) 
 Mwenyekiti wa Timu ya SAM wilaya  ya Iringa Bw. Ngole Mwangosi  akisoma ripoti yao katika mkutano wa marejeo ya mradi wa ushiriki wa wananchi katika usimamizi wa maliasili (CEGO)

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mheshimiwa Richard Kasesela akihitimisha mdahalo kwa kutoa maoni yake juu ya mada zilizojadiliwa na washiriki kutoka serikalini, wadau wa maliasili na wananchi wa mkoa wa Iringa.
Serikali imepewa changamoto ya kutekeleza kikamilifu sheria za Mazingira, Maliasili na Wanyamapori kwa lengo la kupunguza au kumaliza kabisa matatizo yatokanayo na kutofuatwa kwa sheria hizo.
Changamoto  hiyo imetolewa na Timu ya Wanasheria watetezi wa Mazingira kwa vitendo (LEAT) wakati wa mdahalo maalum wa viongozi wa Serikali, wananchi na wadau wa Mazingira, Maliasili na Wanyapori Mkoa wa Iringa. Mdahalo huo ulifunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi.Amina Masenza.
Akizungumza katika Mdahalo huo wa marejeo ya Mradi wa Ushiriki wa wananchi katika Usimamizi wa Maliasili (CEGO) wilaya za Iringa na Mufindi, Mkurugenzi Mtendaji wa LEAT, Dkt. Rugemeleza Nshala amesema licha ya mapungufu kidogo ya sheria hizo lakini zinao uwezo wa kulisaidia Taifa kuondokana na kero za matumizi yasiyo endelevu ya maliasili misitu na wanyama pori.
Awali, Mkuu wa wilaya Iringa amesema Mkoa wa Iringa unakabiliwa na changamoto kubwa ya kilimo cha mabondeni maarufu kama vinyungu na ugumu wa kuwaondoa watu hao unakuja pale inapokosekana shughuli mbadala watakayoifanya ili iwaingizie kipato.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, amesema juhudi za LEAT kutoa elimu kwa Wananchi ni nzuri kwa sababu zinasaidia kupunguza migogoro kati ya wakulima na wafugaji.
Mhadhiri Mwandamizi Chuo kikuu cha kilimo Morogoro (SUA) Dk. Gimbage Mbeyale katika mdahalo huo alisema kuwa mabadiliko ya tabia ya nchi ni moja ya changamoto zinazokwamisha kuwepo kwa utunzaji na umuduji dumivu wa rasilimali misitu na wanyamapori.
Dk. Mbeyale alisema kuwa changamoto hizo zinasababishwa na uvunaji usiozingatia mpango wa usimamizi misitu sambamba na ongezeko la watu nchini kwa asilimia 3.2 toka milioni 11 kwa mwaka 1960 hadi milioni 56 kwa mwaka 2016.
“Migogoro kati ya mamlaka za hifadhi na wananchi (wakulima na wafugaji) ni changamoto za kuwepo kwa utunzaji na umuduji dumivu wa rasilimali misitu na wanyamapori nchini Tanzania” alisema Dk. Mbeyale
Naye msimamizi wa sekta ya Uchumi na Uzalishaji kutoka ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Leo Mavita, alisema kuwa kiini cha changamoto katika utunzaji na umuduji wa rasilimali misitu na wanyamapori ni kuwa na uwezo wa kuchanganua na kuelezea mahusiano yake na jamii na uchumi wake.

No comments:

Post a Comment