Saturday, April 8, 2017

TIMU YA SAM YA WILAYA YA MUFINDI YAFANYA ZIARA YA KUTATHMINI UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA USIMAMIZI WA MALIASILI KATIKA VIJIJI VYA MRADI.


Wajumbe wa Timu ya SAM ya Wilaya ya Mufindi wakifanya mahojiano na uongozi wa kijiji cha Igombavanu juu ya usimamizi wa maliasili za kijiji hicho


Wajumbe wa Timu ya SAM ya Wilaya ya Mufindi wakifanya mahojiano na uongozi wa kijiji cha Mapogoro  juu ya usimamizi wa maliasili za kijiji hicho
Mjumbe akibainisha changamoto za usimamizi wa maliasi katika kijiji cha Ikangamwani
Mwenyekiti wa Timu ya SAM wilaya ya Mufindi Bw. Clemence Mwapelwa akiitambulisha Timu ya Ufuatiliaji wa Ufuatiliaji jamii kwa uongozi wa kijiji cha Ikangamwani

Wajumbe wa Timu ya SAM wakifanya tathmini ya pamoja juu ya mafanikio na changamoto za usimamizi wa maliasili kutokana na ziara zilizofanyika katika vijiji vya Igombavanu, Idumlavanu, Ikangamwani na Mapogoro
Timu ya SAM ya Wilaya ya Mufindi yatembelea vijiji vya mradi vinne ambayo ni Igombavanu, Mapogoro, Idumlavanu na Ikangamwani,  ili kufanya tathmini ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za usimamizi wa maliasili kuanzia ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji.


Pia Timu hiyo ililenga kupima matokeo ya utekelezaji wa shughuli za mradi ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya jinsi halmashauri ya wilaya ilivyotekeleza mapendekezo ya Timu hiyo kama yalivyowasilishwa mwaka jana 2016.


Katika ziara hii Timu iliweza kukutana na baadhi ya wajumbe wa Kamati za maliasili za vijiji, Halmashauri za vijiji, Timu ndogo za SAM za vijiji, na Kamati za uchumi na fedha.


Lengo la kukutana na wajumbe hawa ni kuwahoji na kutoa mrejesho ambao utaisaidia Timu ya SAM ya wilaya kulinganisha kilichopo kwenye nyaraka na kinachotetendeka katika vijiji husika.


Taarifa itakayokusanywa na Timu hii itataja mambo ambayo yatahitaji muitikio kutoka kwa halmashauri za vijiji na halmashauri ya wilaya.


Ripoti itataja mafanikio na changamoto ambazo zimegunduliwa na timu ya SAM ya wilaya, ambazo zitawasilishwa mbele ya Mkurugenzi, Mkuu wa wilaya na Watendaji wakuu wa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi. 

No comments:

Post a Comment