Tuesday, February 21, 2017

VIKUNDI VYA LEAT VYA SANAA KIJIJI CHA MAPOGORO NA MFYOME KATIKA UELIMISHAJI NA UHAMASISHAJI JAMII JUU YA USHIRIKI WA WANANCHI KATIKA USIMAMIZI WA MALIASILI


Katika picha ni kikundi cha sanaa mapogoro kilichowezeshwa na LEAT kutoa elimu ya utunzaji mazingira kupitia sanaa

Afisa Habari wa LEAT Bi. Edina Tibaijuka akihamasisha kikundi cha sanaa Mapogoro kuendelea kutoa elimu ya usimamizi wa maliasili kupitia sanaa.

Picha ya pamoja ya kikundi cha sanaa cha Mapogoro na Afisa habari wa LEAT Bi. Edina Tibaijuka

Katika picha ni baadhi ya wanakikundi cha sanaa Mfyome 


Katika kuhakikisha kuwa jamii kubwa inaelimishwa na kuhamasishwa juu ya Usimamizi wa Maliasili, Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo ( LEAT) inatumia vikundi vya sanaa katika wilaya zinazotekeleza  mradi wa Ushirki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili, wilaya za Iringa na Mufindi.

LEAT ina vikundi viwili vya Sanaa ambavyo ni kikundi cha Sanaa Mapogoro kilichopo wilaya ya Mufindi na kikundi cha Sanaa Mfyome kilichopo wilaya ya Iringa. Kikundi cha Sanaa Mfyome kinaundwa na wasanii kutoka vijiji vya Mfyome na Kiwere.





No comments:

Post a Comment