Thursday, September 25, 2014

KAMATI ZA VIJIJI ZA MAZINGIRA ZAFUNZWA JUU YA USIMAMIZI WA MALIASILI KUPITIA UFUATILIAJI UWAJIBIKAJI JAMII.

KAMATI ZA VIJIJI ZA MAZINGIRA ZAFUNZWA JUU YA USIMAMIZI WA MALIASILI KUPITIA UFUATILIAJI UWAJIBIKAJI JAMII.


Timu ya wanasheria watetezi wa mazingira (LEAT) kupitia mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili ( CEGO-NRM) ambao upo chini ya Ufadhili wa Shirika la maendeleo la misaada la watu wa Marekani (USAID) inaendesha mafunzo ya Usimamizi wa Maliasili kwa kupitia dhana ya mfumo wa Ufuatiliaji wa Uwajibikaji jamii

 (UJJ/SAM) katika mkoa wa Iringa, wilaya mbili za Iringa vijijini na Mafinga.

Mafunzo yalianza mnamo mwezi wa nane na yataendelea hadi mwezi wa kumi mwaka 2014. Walengwa wakuu wa mafunzo haya ni Kamati za Mazingira za vijiji kama vile kamati za maliasili, kamati za maji, kamati za matumizi bora ya ardhi, kamati za mipango na fedha, baraza la ardhi na kamati nyingine zinazohusika na mazingira vijijini.

 Hadi sasa LEAT imeweza kuzifikia kamati hizi na kuwapatia mafunzo ambapo mpaka sasa Katika wilaya ya Iringa vijijini LEAT imeweza kuifikia kata ya KIwere na Idodi ambapo  katika kata ya Kiwere wkamati za mazingira za vijiji vya kiwere, Mfyome,Kitapilimwa na itagutwa vimenufaika na mafunzo haya, vilevile katika kata ya Idodi kamati za vijiji za Tungamalenga, idodi zimefikiwa na kuelimishwa wakati kijiji cha Kitisi kikitegemea kufikiwa na Mafunzo haya mwanzoni mwa mwezi wa kumi.

Kadhalika katika wilaya ya Mafinga LEAT imekusudia kuzifikia kata Mbili ambazo ni Igombavanu na Saadani ambapo mpaka sasa LEAT imeweza kuvifikia vijiji vya Igombavanu, uhambila Lugoda lutali na Tambalang’ombe katika kata ya igombavanu wakati katika kata ya Saadani LEAT imeweza kuvifikia vijiji vya Kibada,Mapogolo wakati kijiji cha utosi kikitegemea kufikiwa mwanzoni mwa mwezi wa kumi.

Mafunzo haya yamelenga kuwafikia angalau wajumbe 35 wa kamati za Mazingira kwa kila kijiji na lengo kuu la mafunzo haya ni

 I. Ni kuijengea uwezo jamii kufahamu mwelekeo sahihi wa uwajibikaji jamii.

 II. Kuelewa dhana ya mfumo wa uwajibikaji jamii katika usimamizi wa misitu na wanyamapori.

  III. Pia kuelewa hatua tano za mchakato wa mfumo wa uwajibikaji jamii ikwa ni pamoja na mpango wa mgawanyo wa rasilimali, usimamizi wa matumizi, usimamizi wa uadilifu na usimamizi wa uangalizi.

 Vilevile mafunzo ya ufuatiliaji na usimamizi wa uwajibikaji wa jamii yanalenga kuongeza uelewa juu ya zana za uwajibikaji na usimamizi wa jamii kwa kufuatilia kila hatua ya mchakato.

 Hivyo basi ufualiaji wa uwajibikaji jamii unawezesha watoa huduma kwa jamii kutoa ufafanuzi, uthibitisho na uhalalisho juu ya mgawanyo wa raslimali za umma, utekelezaji wake na ufanisi/utendaji wake. Lengo ni kuhakikisha kuwa viongozi wa serikali pamoja na watoa huduma wote wanawajibika na wanawajibishwa ipasavyo pale wanaposhindwa kufikisha huduma muhimu kwa jamii kama walivyoorodhesha katika mpango mkakati, Mpango mwaka na bajeti ya Mwaka ili kuweza kufikia haki za msingi za binadamu/mwananchi.

 

No comments:

Post a Comment