Wednesday, November 9, 2011

MALALAMIKO YA WANANCHI WA MTAA WA YOMBO MAKANGARAWE JUU YA KERO ZITOKANAZO NA UJENZI WA BAA KATIKATI YA MAKAZI YA WATU

UTANGULIZI

Chama cha Wanasheria Watetezi wa Mazingira (LEAT) kilipokea malalamiko kupitia Barua ya TAREHE 29.09.2011 kutoka kwa wananchi wa Yombo MAKANGARAWE kuhusu kero zinatokana na uwepo wa Baa na nyumba ya kulala wageni “Guest House” ijulikanayo kama KB METRO PUP iliyotajwa kumilikiwa na Bwana Lugano Kikoti ambayo imejengwa katikati na makazi ya watu.

Kimsingi malalamiko haya yaligusia mambo makuu wawili;

i. Kelele zitokanazo na muziki unaopigwa na baa hiyo hasa wakati wa usiku na kuwa kero kubwa kwa wananchi wanaoishi jirani na baa hizo na kushindwa kupumzika. Vilevile wafanyakazi na wanafunzi kushindwa kusoma kutokana na kelele nyingi zinazotokana na muziki unaokuwa ukiendelea KB METRO PUB.

ii. Suala la uharibifu wa mazingira uliofanywa na Baa hiyo baada ya kuziba iliyokuwa njia kuu au mbondo wa maji jambo linalopelekea kutokea kwa mafuriko makubwa wakati wa masika. Suala hili pia lilitajwa kuharibu nyumba zilizopo karibu na mkondo huo wa maji kiasi cha kuhatarisha usalama wa waishio katika nyumba hizo kutokana na mmomonyoko unaosababishwa na maji yanayojaa wakati wa mvua ikiwa ni matokeo ya kuzibwa kwa mkondo wa maji. Vilevile kwa mujibu wa malalamiko suala hili limekuwa chanzo kikuu cha milipuko ya magonjwa yaa mara kwa mara kutokana na maji yaliyotuama kuwa mazalia ya mbu na mkusanyiko wa uchafu.

Wananchi hawa tayari walikwishafanya juhudi mbalimbali katika kutafuta suluhisho la tatizo hili, na kuripoti katika Mamlaka zfuatazo (LEAT ina nakala ya barua):-

1. Ofisi ya Serikali za Mitaa

2. Kituo cha Polisi Makangarawe

3. Kituo cha Polisi Chang’ombe

4. Baraza la Usuluhishi la Kata ya Makangarawe

5. Ofisi ya Mtendati Kata-Makangarawe

6. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam

Kwa upande wa mlalamikiwa ilielezwa kuwa alijibu malalamiko ya wananchi kwa kutoa NOTISI iliyopokelewa na wananchi tarehe 17.09.2011 kupitia Wakili wake ‘ALEX $ SAMWEL CORPORATE ADVISORY SERVICES’ abayo pamoja na mambo mengine inataja hasara ya Kiasi cha Shilingi Milioni 50 ilyotokana na kilichotajwa kuwa ni kuzuia uendeshaji mzuri wa biashara unaofanywa na wananchi HIVYO kuwataka wananchi hao kumlipa mmliki wa Baa hiyo kiasi cha Shilingi 50 MILIONI kama fidia la sivyo suala hilo litafikishwa katika vyombo vya sheria.

JUHUDI ZA ZILIZOFANYWA NA LEAT

Baada ya kupokea malalamiko hayo LEAT ikiwa taasisi isiyi ya kiserikali inayojishughulisha na usimamizi wa mazingira na haki za binadamu ilifanya mambo yafuatayo:

i.Baada ya LEAT kulipokea suala hili ililifikisha moja kwa moja katika Mamlaka ya serikali inayosimamia mazingira, Baraza la Usimamizi wa Mazingira Tanzania (NEMC) kwa Barua ya Tarehe 04.10.2011 ikiwa ni TAARIFA kwa mamlaka hiyo kama chombo chenye mamlaka na usimamizi wa mazingira Tanzania. Vilevile LEAT iliiomba NEMC kutoa mwakilishi ili kuambatana na timu ya Mwanasheria wa Mazingira pamoja na Waandishi wa Habari katika ziara ya kujiridhisha na malalamiko ya wananchi na kuona hali halisi.

ii. LEAT pamoja na timu ya waandishi wa habari wa magazeti ya MAJIRA na MWANANCHI walifanya ziara katika eneo husika Tarehe 07.10.2011 na kushudia hali halisi pamoja na kufanya mahojiano ya msingi na wawakilishi wa waathirika wa tatito lililo mezani. Ziara hii ilitoa picha halisi ya kilichoelezwa katika barua za malalamiko kwani kimazingira Baa hiyo ipo katikati ya makazi ya watu na kuwa suala la pili la mkondo wa maji ni kweli kabisa linajidhihirisha.

iii. LEAT baada ya kujiridhisha na malalamiko ililifikisha suala kwa jamii hilo kupitia magazeti la Majira Tarehe 09 na 10/10/2011 na kuripoti NEMC ambao hawakuweza kuwepo katika ziara ya kutembelea eneo husika. Hatahivyo NEMC walishauri wananchi wenyewe kulifikisha suala hilo NEMC ushauri ambao LEAT iliufikisha kwa walalamikaji.

TATIZO LA MSINGI NA MAPENDEKEZO

Pamoja na malalamiko mengi kuripotiwa LEAT imegundua matatizo makuu mawili na mapendekezo yake kama ifuatavyo:-

Kwanza, Baa ya KB METRO PUB imejengwa katikati ya makazi ya watu jambo lililoibua kero nyingine nyingi. Endapo Baa hii itaondolewa katika eneo husika kero nyingine nyingi zikiwemo za kelele za muziki, danguro linalosemekana kewepo, taka zinatupwa eneo hilo na mgomgano huu baina ya mmiliki na wananchi vitakwisha.

Pili, Suala la kuzua mkondo wa maji wa asili, hili pia litaweza kusuluhishwa na pendekezo lililotajwa hapo juu kwani uzibuaji wa mkondo asili wa maji utategemea kubomolewa kwa sehemu ya ukuta wa Baa hiyo. Kwa kuwa NEMC waliahidi kulifanyia kazi suala hili baada ya kupata malalamiko ya Wananchi tunategemea suala hili kulingana na mazingira yake litafanyiwa kazi.

Katika kutafuta suluhu LEAT imfanikiwa kufanya taratibu za awali ikiwemo kutoa Taarifa NEMC kikiwa ni chombo chenye Mamlaka kisheria kusimamia mazingia nchini. Vilevile LEAT imetumia vyombo vya habari kupaza sauti hizi za watanzania, Gazeti la Majira la Tarehe 9/10/2011 Ukurasa wa 5 linaripoti. LEAT pia ipo katika mchatako wa kuripoti suala hili kwa Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia Jeshi la Polisi hasa kwa suala la kupiga kelele za muziki katikati ya makazi ya watu usiku kucha.

MENGINEYO

Katika utekelezaji wa shughuli hii yameibuka malalamiko mengi ya aina hiyo kutoka katika mitaa mbalimbali hapa jijini Dar es Salaam ikiwemo mtaa huo huo wa Makangarawe ambapo Baa ya BATOTOZI km Night Club imeripotiwa.

Mwisho LEAT itaendelea kuwa na wananchi katika harakati za kutetea haki zao za kimazingira ili wapate mazingira mazuri ya kuishi, ikiwa ni haki ya kisheria ‘Haki ya Kuishi’.

No comments:

Post a Comment